• Breaking News

    ..

    ..

    Monday, 15 January 2018

    TRL yabadili ratiba za safari

    Na Stahmil Mohammed
    Kampuni ya reli Tanzania(TRL)imeamua kuendelea kutoa huduma  ya usafirishaji wa abiria kuanziaDodoma kwenda kigoma,mwanza na Mpanda hadi hali ya miundombinu itakapokuwa vizuri baada ya ukarabati kukamilika.Image result for TREN

    Hayo yamesemwa Leo na Kaimu Naibu Mkurugenzi wa TRL Focus Makoye Saloni alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na mabadiliko ya safari za treni Mara baada ya kuharibiwa  kwa miundombinu ya reli  ya kati ya Stesheni za kilosa na Gulwe kutokana na mafuriko ya mvua zilizonyesha maeneo hayo.

    Akitaja ratiba ya usafiri huo kuanzia Dodoma na muda wa safari Bw.Makoye amesema treni itaanza safari Dodoma itatoka Saa moja usiku Sikh ya jumanne na ijumaa kwenda kigoma  Mpanda na  kuwasili mwanza saa 12 jioni siku ya jumatano na  mpanda sa 12:00 jioni na kigoma saa 12:30 jioni.

    Aidha Treni kutoka Mpanda ,mwanza na kigoma zitatoka huko siku za jumapili na alhamisi tu.Treni hiyo itatoka saa 1:00 asubuhi mwanza inatoka saa 2:00 asubuhi na kigoma inatoka saa 1:30 asubuhi hivyo treni hizo zinafiks Dodoma siku ya jumatatu na ijumaa saa 1:00 asubuhi.wakati huo huo treni pekee ya kutoka Tabora kwenda Mpanda itafanya safari zake siku ya jumanne,Alhamisi na jumapili na itatoka Mpanda kurejea Tabora katika siku za jumatatu,jumatano,jumamosi na itakuwa ikiondoka Tabora saa 12 asubuhi na kuwasili Mpanda saa 12:32 jioni na itaondoka Mpanda kurejea  Tabora saa 1:00 asubuhi na kuwasili saa 12:38 jioni.Image result for TREN

    Kwa upande wake Meneja wa usalama wa reli Gakwi Michael amesema tabia ya watu kulima pembezoni mwa reli wamechangia kwa kiasi kikubwa hivyo amewataka watu kwenye Tania hizo kuacha Mara moja.

    Hata hivyo uongozi wa TRL bado unaendelea kusimamia kazi ya ukarabati wa eneo lililoharibika kati ya kilosa na Gulwe.

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI