Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo nchini (HESLB), Abdul Razaq
Badru amesema kuwa, kuanzia mwaka jana mpaka sasa wamefanikiwa kuwapata
wadaiwa sugu 26,000 wa mikopo ya elimu ya Juu na bado wanaendelea na
msako wa kuwatafuta. 

Mkurugenzi huyo wa (HESLB) amewapongeza sana waajiri kwa kutoa
ushirikiano wao kwa kuendelea kuwasilisha makato ya mishahara kwa
waajiriwa wao wanaodaiwa na bodi hiyo kwa asilimia 15 kama sheria
inavyosema japo bado kuna waajiri hawajatoa ushirikiano kwani bado
hawajaanza kuwakata kabisa waajiriwa wao.
Abdul Razaq Badru ameendelea kufafanua kuwa kuanzia Januari nane mwaka huu wataanza kufuatilia taarifa za waajiriwa katika taarifa zao za kibenki ili kubaini nani ni mnufaika wa mkopo ili kuanza kurudisha fedha hizo katika bodi ya mikopo na kuweza kuendelea kunufanisha wahitaji wengine.
Mpaka sasa bodi ya mikopo inadai jumla ya bilioni 285 kwa wadaiwa wote, huku mkurugenzi wa bodi hiyo akibainisha kuwa wanataka kufikia mwezi wa saba wawe na wastani wa ukusanyaji wa madeni hayo kwa mwezi uwe umefika bilioni 17 kutoka bilioni 13 kama ilivyokuwa awali.
Abdul Razaq Badru ameendelea kufafanua kuwa kuanzia Januari nane mwaka huu wataanza kufuatilia taarifa za waajiriwa katika taarifa zao za kibenki ili kubaini nani ni mnufaika wa mkopo ili kuanza kurudisha fedha hizo katika bodi ya mikopo na kuweza kuendelea kunufanisha wahitaji wengine.
Mpaka sasa bodi ya mikopo inadai jumla ya bilioni 285 kwa wadaiwa wote, huku mkurugenzi wa bodi hiyo akibainisha kuwa wanataka kufikia mwezi wa saba wawe na wastani wa ukusanyaji wa madeni hayo kwa mwezi uwe umefika bilioni 17 kutoka bilioni 13 kama ilivyokuwa awali.
No comments:
Post a Comment