Jana ilikuwa ni siku ya kihistoria ya soka la nchi ya Saudi Arabia
baada ya wanawake nchini humo kuhudhuria mechi ya soka kwa mara ya
kwanza.

Ruhusa ya wanawake kuingia uwanjani ilitolewa mwezi Oktoba mwaka jana na Mtawala wa sasa wa nchi hiyo (Crown Prince Mohammad Bin Salman Al Saud) ikiwa ni sehemu ya mabadiliko makubwa yanayofanyika nchini humo yanayolenga kuleta haki na usawa kati ya mwanamke na mwanaume katika baadhi ya maeneo.

Alhamisi ijayo pia wanawake watapata nafasi ya kuhudhuria mechi kwenye uwanja wa Prince Mohammed bin Fahd mjini Dammam wakiketi na familia zao kama ilivyokuwa jana. Mwaka jana pia serikali ilitoa ruhusa ya wanawake kuanza kuendesha gari katika shughuli zao mbalimbali za kila siku.
No comments:
Post a Comment