Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya
Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akimuuliza maswali Mhandisi wa
Jeshi la Polisi, Mrakibu Pascal MacORWA (kushoto), alipotembelea eneo la
Tunguu lililovamiwa na wananchi, ambalo mmiliki halali ni jeshi la
Polisi. Wakwanza kulia ni Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kusini
Unguja,Makarani Khamis na watatu kulia ni Mkuu wa mkoa huo, Hassan
Khatib Hassan.Naibu Waziri yuko Visiwani Zanzibar kwa ziara ya kikazi.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kusini
Unguja, Makarani Khamis , akitoa maelezo kwa Naibu Waziri Wizara ya
Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, juu ya eneo la Tunguu
lililoko Mkoa wa Kusini Unguja ambalo ni mali ya Jeshi la Polisi, hivi
sasa likimilikiwa na wananchi kinyume cha sheria.Kushoto ni Mkuu wa mkoa
huo, Hassan Khatib Hassan. Naibu Waziri yuko Visiwani Zanzibar kwa
ziara ya kikazi.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya
Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akionyeshwa na Mhandisi wa Jeshi
la Polisi, Mrakibu Pascal MacORWA, ramani ya moja ya maeneo
yanayomilikiwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Kusini Unguja wakati wa ziara
ya naibu waziri kukagua maeneo yanayotarajiwa kujengwa vituo vya polisi
mkoani hapo.Kulia ni Mkuu wa Mkoa huo,Hassan Khatib Hassan. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja,
Hassan Khatib Hassan, akizungumza na Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya
Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni baada ya kukagua makazi ya askari
polisi yanayoonekana pichani, yaliyopo eneo la Machui, lililopo Mkoa wa
Kusini Unguja.Naibu Waziri yupo Visiwani Zanzibar kwa ziara ya kikazi ya
kukagua maeneo yanayotarajiwa kujengwa vituo vya polisi na makazi ya
askari.Kulia ni Kiongozi wa Chama cha Mapinduzi mkoani hapo.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja,
Hassan Khatib Hassan, akizungumza na Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya
Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni baada ya kukagua eneo yalipojengwa
maduka ya biashara ambayo wamiliki wamenunua viwanja hivyo vya Jeshi la
Polisi kinyume na utaratibu. Naibu Waziri yuko Visiwani Zanzibar kwa
ziara ya kikazi.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya
Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akisalimiana na viongozi wa Mkoa
Kusini Unguja alipowasili leo mkoani hapo kwa ziara ya kikazi ya
kukagua maeneo yanayotarajiwa kujengwa vituo vya polisi na makazi ya
askari.Kulia ni Kiongozi wa Chama cha Mapinduzi mkoani hapo.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
No comments:
Post a Comment