Kijana mmoja aitwae Shazili Saidi Mkuchi mkazi wa Mtwara mwenye umri wa
miaka 26, anatafutwa na polisi kwa tuhuma za kumuua mama yake mzazi Bi.
Amina Chuwalila kwa kumkata na panga.
“Kama angemkosa mama, basi kifo hiki kingekuwa cha kwangu maana na mimi nimetajwa kuwa nilikuwa nashirikiana na mama yetu kumroga yeye”, amesema kaka wa mtuhumiwa Saidi.
Daktari wa kituo cha afya cha Nanguruwe aliyejulikana kwa jina la Dokta Adam amekiri kumpokea mama huyo akiwa amejeruhiwa vibaya, na kwamba tayari alikuwa ameshafariki.
Kamanda wa polisi mkoa wa Mtwara Lucas Mkondya amethibitisha kuripotiwa kwa tukio hilo ambalo limetokea Machi 14, na kuwataka wananchi kusaidia kufanikisha kumpata mtuhumiwa huyo ambaye ametokomea kusikojulikana.
No comments:
Post a Comment