• Breaking News

    ..

    ..

    Friday 23 March 2018

    MJEMA ATOA MBINU KUTOKOMEZA UGONJWA WA KIFUA KIKUU MANISPAA YA ILALA.

    Watanzania wametakiwa kuwa na ushirikiano katika kuhakikisha wanatokomeza ugonjwa wa kifua kikuu ambao umeonekana sio rafiki kutokana na kugharimu maisha ya watu.

    Akizungumza katika maadhimisho ya Ugonjwa wa Kifua kikuu katika Manispaa ya Ilala, Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Sophia Mjema amesema kuwa ugonjwa huo unapaswa kupigwa vita na kila mtu.

    Mhe. Mjema ambaye ni mgeni rasmi katika maadhimisho hayo, amesema kuwa ni vema kila mtu anamlinde mwezake jambo ambalo litasaidia kupunguza idadi ya wagonjwa wa kifua kikuu hapa nchini.

    " Wilaya ya Ilala sasa inatakiwa kuanzisha kampeni ya kutokomeza ugonjwa wa kifua kikuu kwenda kwa mtu mwengine" amesema Mhe.Mjema.

    Ameeleza kuwa kuna baadhi ya watu wamekuwa wakitema mate hovyo, bila kujua kufanya hivyo kunaweza kuchochea ongezeko la ugonjwa wa kifua kikuu kutokana ugonjwa huo unaambukiza kwa njia ya hewa.

    "Imefika wakati kupiga vita vitendo hatarishi kwa afya ikiwemo kuuza vyakula pamoja  matunda ambayo hayajaifadhiwa sehemu salama ili kuepuka magonjwa" amesema Mhe. Mjema.

    Mganga Mkuu wa Ilala amebainisha kuwa kwa mujibu wa shirika la afya duniani, Tanzania inashika nafasi ya sita kuwa watu wenye ugonjwa wa kifua kikuu, huku Afrika ikiwa nafasi ya nne.

    Ameseme kuwa katika Wilaya ya Ilala kuna maeneo ambayo yanaongoza kuwa na wagonjwa wengi wa kifua kikuu ambayo ni Kata ya Buguruni, Ukonga, Kiwalani pamoja na Vingunguti.

    Imeelezwa kuwa kata hizo zinachangia asilimia 80 kwa wagonjwa wenye kifua kikuu ambao wanagundulika takribani 5,000 kila mwaka.

    Manispaa ya Ilala wameadhimisha leo siku ya wagonjwa wa kifua kikuu katika kata ya Mchikichini jijini Dar es Salaam wakiwa na kauli mbiu ya mwaka huu ‘Viongozi tuwe mstali wa mbele kuongoza mapambano ya kutokomeza kifua kikuu’.

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI