• Breaking News

    ..

    ..

    Tuesday 10 April 2018

    Watumishi wa umma walioondolewa kazini warejeshwa

    Chama cha wafanyakazi wa serikali za mitaa Tanzania (TALGWU) kimeishukuru  serikali kuwarudisha kazini watumishi walioajiriwa kabla ya tarehe 20 Mei 2004 ambao waliondolewa kwenye mfumo wa malipo ya mshahara kwa kukosa sifa ya cheti cha kidato cha nne.

    Akizungumza na waandishi wa habari katibu mkuu TALGWU Rashid Mtima amesema anaishukuru serikali ya awamu ya tano kwa kuzingatia mapendekezo yaliyowasilishwa na chama hiko serikalini mnamo tarehe 22 machi mwaka huu.

    Amesema mapendekezo waliyowasilisha serikalini ilikuwa ni kuiomba serikali kuwarudisha kazini  watumishi wote walioondolewa katika utumishi kwa kukosa sifa ya kuwa na elimu ya kidato cha nne.

    Aidha amesema kufikia tarehe 9 april mwaka huu menejimenti ya utumishi wa umma na utawala bora mh. Kapten mstaafu George Mkuchika alitoa kauli ya serikali bungeni Dodoma ya kuwarejesha watumishi hao kazini,walipwe mishahara yao kwa kipindi chote walioondolewa na kuendelea na ajira zao mpaka watakapostaafu kwa mujibu wa sheria.

    Pia ametoa pole kwa wanachama na watumishi wote ambao waliondolewa katika utumishi wa umma kimakosa na waajiri wao kwa kigezo cha kuwa na elimu ya darasa la saba.

    Hata hivyo  Mtima amesema baadhi ya waajiri katika halmashauri mbalimbali katika kutekeleza agizo la menejimenti ya umma ya kuwaondoa watumishi  hao walifanya tafsiri potofu na kuwaondoa watumishi wenye elimu ya darasa la saba walioajiriwa kabla ya tarehe 20  mei 2004 na kupelekea wanachama 7,382 kuondolewa kazini.

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI