• Breaking News

    ..

    ..

    Tuesday, 14 November 2017

    Mambo 9 yaliyojiri bungeni katika kipindi cha maswali na majibu

    Mambo makuu 9 yaliyojiri bungeni katika kipindi cha maswali na mjibu leo Novemba 14 mwaka huu. Ambapo bunge hilo limeongozwa na Naibu Spika wa Bunge, Dkt Tulia Ackson.

    Katika mkutano wa tisa kikao cha sita wabunge mbalimbali waliuliza maswali na kujibiwa na serikali kama ilivyo kawaida, haya ni mambo 9 kwa ufupi yaliyozungumzwa ndani ya Bunge.
    #Makusanyo yatokanayo na kodi za majengo kutoka Halmashauri za Miji, Manispaa na Majiji 30 yaliyokuwa yakisimamiwa na TRA yameongezeka kutoka shilingi bilioni 28.28 mwaka 2015/16 hadi bilioni 34.09 kwa mwaka 2016/17 – Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji.
    #Kodi za majengo kutoka Halmashauri za Miji, Manispaa na Majiji kwa mwaka 2015/16 ilikusanywa na Serikali za Mitaa na mwaka 2016/17 TRA ilianza kukusanya kodi hiyo – Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji.
    #Ongezeko la makusanyo linadhihirisha kuwa, TRA imefanya vizuri zaidi katika kukusanya mapato hayo ikilinganishwa na Halmashauri hizo 30 katika mwaka 2015/2016 – Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji.
    #Katika kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifunzia wanafunzi wenye ulemavu nchini, Serikali imetoa mafunzo kazini kwa walimu 699 wanaofundisha wanafunzi wenye ulemavu wa akili na wenye usonji – Mhe. William Ole Nasha.
    #Wizara ya Elimu inakamilisha uandaaji wa mwongozo wa kufundishia wanafunzi wenye ulemavu wa akili na wenye usonji ambao utasambazwa katika vitengo 349 vinavyopokea wanafunzi hao – William Mhe. Ole Nasha.
    #Mwongozo huo unalengo la kupanua uelewa wa walimu juu ya mbinu za kufundishia, matumizi ya vifaa pamoja na saikolojia ya kufundishia wanafunzi hao – William Mhe. Ole Nasha.
    #Maafisa Maendeleo ya Jamii walikuwa wakitumika kama spare tire katika Halmashauri. Lakini kuanzia sasa tumewapa mwongozo wa kuwafikishia wakurugenzi wao ili waweze kuwatumia – Mhe. Selemani Jafo.
    #Kuanzia sasa mtaona mwenendo tofauti wa utendaji wa Maafisa Maendeleo ya Jamii chini ya Wizara ya Afya pamoja na TAMISEMI ambao wanawasimamia kwa ukaribu – Mhe. Selemani Jafo.
    # Maafisa Maendeleo ya Jamii ndio injini ya mabadiliko katika Halmashauri – Mhe. Selemani Jafo.
    CHANZO BONGO 5.COM

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI