• Breaking News

    ..

    ..

    Thursday, 15 December 2016

    TAKWIMU: VIFO VYA WATOTO VINAVYOSABABISHWA NA MALARIA VIMEPUNGUA NCHINI

    Serikali imezindua ripoti ya utafiti wa afya ya uzazi na mtoto na viashiria vya malaria ya mwaka 2015/16 mapema hii leo jijini Dar es Salaam ikiwa ni awamu ya tatu katika ugonjwa wa malaria ambapo ripoti imeonesha kupungua kwa vifo vya watoto wadogo.meza-kuu

    Akizungumza katika uzinduzi huo Mgeni Rasmi Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu ameipongeza Ofisi ya Taifa ya Takwimu kwa kuaanda ripoti iliyoonesha Taifa kupiga hatua katika utoaji wa huduma ya mama na mtoto.waziri-ummyy

    Waziri Ummy ameeleza kuwa ripoti hiyo itaisaidia Wizara ya Afya na serikali kwa ujumla katika kutathmini na kufuatilia utekelezaji wa mipango endelevu katika huduma za afya hapa nchini ili kuboresha utoaji wa huduma ambazo ripoti imeonesha haikufanya vizuri kutokana na changamoto mbalimbali ambazo ripoti imezibainisha.

    “Ripoti hii imeonesha kuwa bado kuna changamoto katika mimba za utotoni kwani  zimeongezeka ukilinganisha na mwaka 2010 ambapo watoto 23 kati ya mia moja walipata mimba wakiwa na umri mdogo ukilinganisha na sasa watoto 27 kati ya mia moja hupata mimba katika umri mdogo hivyo kuna haja ya jamii kuelimishwa juu ya madhara ya mimba za utotoni”, alisema Waziri Ummy.picha-takwimu

    Ameongeza kuwa kuna haja ya serikali kuangalia upya sheria ya kuruhusu mwanafunzi kuendelea na masomo endapo akipata mimba akiwa shuleni kwani kumzuia kuendelea na masomo ni kupoteza nguvu kazi ya taifa na kuikwamisha serikali kufikia malengo yake ya uchumi wa viwanda.

    Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Dk. Albina Chuwa amesema kuwa iwapo huduma za afya zitaboreshwa zitapelekea ukuaji wa uchumi kwasababu ya uwepo wa nguvu kazi ya uhakika na kuongeza uzalishaji kwa Taifa.dk-chuwa

    Jiunge nasi 

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI