Timu za Ivory Coast na Togo zimeshindwa kutambiana katika michuano ya Kombe la Mataifa barani ‘AFCON’ inayoendelea nchini Gabon baada ya kutoka sare ya bila kufungana mchezo uliochezwa kwenye uwanja wa Stade d’Oyem mjini Oyem.
Mchezo huu umechezwa majira ya saa 1:00 usiku kwa saa za Afrika Mashariki licha ya Ivory Coast kuwa na wachezaji wengi wanaocheza Ligi ya Ulaya wameshindwa kuonesha makali yao dhidi ya Mchezaji mkongwe wa Tongo Emmanuel Adebayo.
Mchezo wa pili unatarajia kuanza saa nne usiku kwa kuzikutanisha timu za DR.Congo watakaowavaa Morroco ambao wanapewa nafasi ya kufanya vizuri katika kundi hilo.
No comments:
Post a Comment