• Breaking News

    ..

    ..

    Wednesday, 15 February 2017

    Meya Ilala kuitisha kikao maalum kwa ajili ya miradi ya Halmashauri hiyo

    Kupitia kikao cha baraza la madiwani la Halmashauri ya Ilala Mstahiki Meya Charles Kuyeko amehaidi kufanya kikao maalum kwaajili ya kuzungumzia miradi ya Halmashauri hiyo ili waweze kukusanya mapato yenye tija kwa Halmashauri hiyo.
    Kauli hiyo ya mstahiki meya imekuja kufuatia mchango wa mbunge wa jimbo la Segerea Bonnah Kaluwa kuitaka Halmashauri kuweka utaratibu utakao walinda bodaboda licha ya kuwafanya wao ndiyo chanzo cha mapato, ukizingatia serikali imesitisha ajira kwa sasa.
    Katika hatua nyingine baraza hilo limezungumzia matokeo mabovu ya kidato cha nne kwa shule za Mbondole, Kitonga na Nyeburu ambapo Mbunge wa jimbo la Ukonga Mwita Waitara amezitaja sababu za miundombinu ndiyo iliyopelekea wanafunzi wa shule hizo kufeli kwani zipo mbali na wanafunzi wengi wanao soma hapo, sababu inayopelekea wengi kutokwenda shule kwa kukosa nauli, kwakuwa usafiri mkubwa unatumika ni bodaboda kutokana na miundombinu isiyo rafiki.
    Pia Mbunge huyo amewataka wazazi kutoichukulia vibaya dhana ya elimu bure kwa kuitupia mzigo serikali kwani nao wanapaswa kushiriki kwenye shughuli za maendeleo ya elimu ikiwemo kuchangia ujenzi wa uzio na mambo yenye tija kama hayo.

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI