Naibu
Kamishna wa TRA, Bw. Qandiyay Akonaay, akitoa maelezo namna Idara ya
Forodha inavyotekeleza majukumu yake katika Mpaka wa Kasumulu/Songwe
(Tanzania na Malawi) baada ya kutembelewa na Ujumbe wa Serikali
ukiongozwa na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Bi. Amina
Khamis Shaaban, ukiwahusisha Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara
na Uwekezaji, Prof. Adolf Mkenda na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya
Ndani ya Nchi, Balozi Hassan Simba Yahya.
Baadhi ya maafisa wa Wizara ya
Fedha na Mipango, Wizara ya Viwanda, Biashara na uwekezaji, na Mamlaka
ya mapato Tanzania TRA, wakifuatilia kwa makini maelezo yaliyokuwa
yakitolewa wakati wa ziara ya ujumbe wa Serikali ukihusisha Makatibu
wakuu wa Wizara hizo na Taasisi zake, walipotembelea na kukagua shughuli
za forodha na uhamiaji zinazoendelea katika mpaka huo wa Tanzania na
Malawi, eneo la Kasumulu.
Afisa
Forodha wa mpaka wa Tanzania na Malawi Mkoani Mbeya-Kasumulu, Bw.
Lenny Mkolla (Wa nne kulia) akitoa maelezo kuhusu mpaka huo baada ya
kutembelewa na Ujumbe wa Serikali ukiongozwa na Naibu Katibu Mkuu
Wizara ya Fedha na Mipango Bi. Amina Khamis Shaaban (wa pili kulia),
Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji Prof. Adolf
Mkenda (wa tatu kushoto) na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani
ya Nchi, Balozi Hassan Simba Yahya (hayupo pichani), Wilayani Kyela
Mkoani Mbeya.
Naibu
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Balozi Hassan Simba
Yahya (wa kwanza kulia), akitoa ushauri kwa uongozi wa mpaka wa
Kasumulu/Songwe (Tanzania na Malawi), upande wa Tanzania, Wilayni Kyela
Mkoani Mbeya, namna ya kuboresha utendaji kazi mpakani hapo ili
kuboresha biashara na kuongeza mapato ya Serikali. Wengine ni Katibu
Mkuu wa Wizara ya Viwanda Biashara na Uwekezaji Prof. Adolf Mkenda (wa
pili kulia), Mrakibu Mwandamizi wa Uhamiaji-Kasumulu, Bw. John Gillagiza
(wa kwanza kushoto), walipotembelea mpaka huo..
Katibu
Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji Prof. Adolf Mkenda
(kushoto) akisisitiza kauli mbiu ya “siku moja! mzigo umetoka” kwa
watumishi wa Idara ya Forodha katika mpaka wa Kasumulu/Songwe (Tanzania
na Malawi), baada ya ujumbe wa Serikali ukiongozwa na Naibu Katibu Mkuu
wa Wizara ya Fedha na Mipango Bi. Amina Khamis Shaaban (kulia)
ulipotembelea na kukagua mpaka huo wilayani Kyela mkoani Mbeya.
Mfanyabiashara
ndogo ndogo katika Mpaka wa Kasumulu/Songwe (Tanzania na Malawi,
wilayani Kyela mkoani Mbeya, Bw. Maombi Simon, akiwa anafuatilia ziara
ya Ujumbe wa Serikali kutoka Wizara tatu za Fedha, Uwekezaji na Mambo ya
ndani, uliotembelea mpaka huo kukagua shughuli za idara ya Forodha na
Uhamiaji, mpakani hapo.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda,
Biashara na Uwekezaji, Prof. Adolf Mkenda (wa kwanza kushoto), Naibu
Kamishna wa TRA, Bw. Qandiyay Akonaay (wa pili kushoto), na wajumbe
wengine wakiwasili katika Ofisi za Idara ya Uhamiaji katika Mpaka wa
Kasumulu/Songwe, (Tanzania na Malawi), ili kukagua shughuli za forodha
katika mpaka huo, wilayani Kyela Mkoani Mbeya.
(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-WFM)
……………………………………………………………………………
Benny Mwaipaja-WFM, Kyela
KATIBU Mkuu Wizara ya Viwanda,
Biashara na Uwekezaji, Prof. Adolf Mkenda, amesema kuwa Serikali
inathamini mchango wa sekta ya biashara katika kukuza uchumi na
maendeleo ya nchi hivyo itaendelea kuweka mazingira mazuri ya ufanyaji
biashara na uwekezaji.
Prof. Mkenda amesema hayo
wilayani Kyela Mkoani Mbeya, wakati ujumbe wa Serikali ukiongozwa na
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bi. Amina Khamis
Shaaban, ulipotembelea mpaka wa Tanzania na Malawi-Kasumulu, ili
kujionea utendaji kazi wa Idara ya Forodha na Uhamiaji katika mpaka huo
wa Kasumulu/Songwe.
Amesema kuwa Serikali inapohimiza
ulipaji na kusimamia ulipaji kodi haina maana kwamba inawachukia
wafanyabiashara, bali inatambua umuhimu wa sekta hiyo katika uchumi wa
Taifa na kutoa wito kwa idara za Serikali zilizoko Mipakani kuboresha
mazingira ya utoaji huduma ili kurahisisha biashara.
“Tunatakiwa kuondoa vikwazo vya
ufanyaji biashara ikiwemo ucheleweshaji wa mizigo inayovushwa katika
mipaka yetu kwa kuwa hatua hiyo itaongeza ufanisi wa Bandari ya Dar es
Salaam na kuzivutia nchi nyingi zaidi kutumia Bandari hiyo” Aliongeza
Profesa Mkenda
Amewaonya watendaji wa Serikali
walioko katika mipaka yote ya nchi, kuacha kufanyakazi kwa mazoea na
kusisitiza kuwa wale wote watakaoshindwa keendana na kasi ya Serikali ya
Awamu ya Tano ni afadhali wapishe kwa hiari yao.
Kwa Upande wake, Naibu Katibu
Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bi. Amina Khamis Shaaban, amesema
kuwa Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Taifawa miaka Mitano, unahitaji
zaidi ya Shilingi Trilioni 107 na kwamba upatikanaji wa fedha hizo
utahitaji mazingira bora ya kukuza uchumi wa nchi ikiwemo mazingira
mazuri ya ufanyaji biashara mipakani
“Serikali itazifanyiakazi
changamoto mlizozisema kama vile upungufu wa wafanyakazi, vitendeakazi
na nyumba za watumishi, lakini wito wangu kwenu muendelee kufanyakazi
kwa pamoja, mshirikiane kwa kuongeza nguvu ili kuongeza mapato ya
Serikali” alisisitiza Bi. Amina Khmis Shaaban
Naye Naibu Katibu Mkuu wa Wizara
ya Mambo ya ndani ya Nchi, Balozi Hassan Simba Yahya, amelitaka jeshi la
polisi hususan kikosi cha usalama barabarani kupunguza urasimu wakati
wa kutekeleza majukumu yao wanapokutana na magari yaendayo masafa marefu
nje ya mipaka ya Tanzania, wasiyacheleweshe njiani bila sababu za
msingi.
Kwa upande mwingine, Naibu
Kamishna wa Mamlaka ya Mapato Tanzania-TRA, Bw. Qandiyay Akonaay,
ameeleza kuwa TRA imeanzisha mfumo wa kufuatilia mwenendo wa mizigo
inayosafirishwa kutoka Bandari ya Dar es Salaam, kwenda nchi jirani,
hatua ambayo imeboresha kwa kiasi kikubwa ucheleweshaji wa mizigo na
kwamba hatua hiyo pia imeongeza mapato ya kodi ya Serikali
No comments:
Post a Comment