• Breaking News

    ..

    ..

    Saturday 29 April 2017

    Soko la mbao Shinyanga lateketea kwa moto

    MABANDA 13 yanayouza mbao katika soko la Kambarage mjini Shinyanga yameteketea kwa moto na kusababisha hasara ya mamilioni ya fedha kwa wafanyabiashara wa mbao.

    Tukio hilo limetokea jana saa 5.30 usiku, ambapo moja ya banda ndio lilianza kuungua na hatimaye yote yakashika kasi kuwaka na kuteketeza mbao zote.

    Mmoja wa walinzi wa mabanda hayo Faustine Mapuli, alisema wakati akizungukia lindo lake gafla akaona moto ukiwaka kwenye banda moja na hivyo kuwaita wenzake na kuaanza kuuzima kwa kuumwagia michanga, lakini walipomwaga maji ndipo ukalipuka na kuwazidi.

    Alisema baada ya kuwazidi walipiga simu kwa wamiliki wake ambao ndio wakatoa taarifa Jeshi la Zimamoto ambao walifika eneo la tukio kujitahidi kuuzima lakini wakati huo mbao zote na mashine za kulandia zikiwa zimeshaungua kutokana na moto huo kuwa mkubwa.

    Naye mmoja wa wamiliki wa mabanda hayo Mosesi Mizungu, alisema kutokana na tukio hilo amepata hasara zaidi ya Sh. Milioni 15 jna kupoteza nyaraka mbalimbali za biashara yake zikiwamo za mikopo na madeni ambayo anadai wateja wake

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI