• Breaking News

    ..

    ..

    Thursday, 6 April 2017

    Temba: Kila msanii wa TMK alikuwa anapata nafasi kutokana na kufanya vizuri kwa mashabiki



    Mh Temba amedai kuwa hapo zamani kundi la TMK Wanaume Family lilikuwa haliachii kazi za wasanii wao kwa nafasi bali walikuwa wanampatia nafasi msanii yeyote aliyekuwa anakubalika katika kipindi husika.

    Rapper huyo amekiambia kipindi cha On The Eight cha ETV, msanii yoyote ambaye wimbo wake umepokelewa vizuri basi atapewa nafasi zaidi kwa kipindi hicho hata kwa kuachia albamu ili kuwafurahisha zaidi mashabiki wao.
    Temba ameongeza kuwa hata wazo la kuanzisha kituo cha Mkubwa na Wanawe lilianzia kwake kutokana na matatizo kadhaa yaliyowahi kujitokeza huko nyuma kwa baadhi ya wasanii wenzao kujitoa kwenye kundi kwa madai walikuwa wanadhulumiwa na Said Fella.
    Kwa sasa Temba na Chege wanafanya vizuri na wimbo wao mpya ‘Go Down’ ambapo video yake mpaka sasa imeshatazamwa mara 533k kwenye mtandao wa Youtube

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI