Baraza la wadhamini wa klabu ya
Simba linaloongozwa na Khamis Kilomoni limesema kwamba hautambui mkutano
mkuu wa klabu hiyo unaotarajiwa kufanyika mwezi ujao.
Akiongea mbele ya waandishi wa
Habari leo hii,katibu wa baraza la wadhamini hao Fikilini Mkwabi alisema
kwamba wao hawautambui mkutano huo kwani viongozi ambao wameandaa
mkutano hawana mamlaka ya kuchukua jukumu hilo la kuitisha mkutano mkuu.
Alisema kwamba kipindi hiki si
kipindi cha kujadili hoja ya mabadiliko wakati viongozi wakuu wa klabu
waliochaguliwa na wanachama wanatuhumiwa na vyombo vya sheria.
Nao baadhi ya wanachama wa klabu
hiyo ya Simba kwa upande wao wameungana na baraza hilo la wadhamini kwa
kutoutambua mkutano mkuu kutokana na viongozi waliopo madarakani kudai
hawapo kihalali.
Mmoja wa wanachama hao
aliyejitambulisha kwa jina la Said Bedui amesema kuwa kwa upande wao
wamebaini kuwa mkutano huo una lengo la kufanya mabadiliko ya katiba ili
klabu hiyo iwe katika mfumo wa hisa ambapo kwao jambo hilo hawalitaki
kwa kuwa wanachama hawana elimu ya kutosha juu ya mfumo huo
No comments:
Post a Comment