Katibu wa Kamati ya Kuzuia
Usafirishaji Haramu wa Binadamu , Seperatus Fella, akizungumza na wadau
kutoka taasisi zinazojihusisha na kupambana na biashara hiyo
waliokutana katika jijini Dar es Salaam leo, ili kujadili mikakati ya
kutokomeza biashaara hiyo nchini. Kikao hicho kimefanyika katika ukumbi
wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Afisa uchunguzi Sekretarieti ya
Kuzuia na Kupambana na Biashara Haramu ya Usafirishaji Binadamu, Ahmed
Mwendadi, akifafanua jambo kwa wadau kutoka Taasisi zinazopambana na
biashara hiyo waliokutana jijini Dar es Salaam, ili kujadili mikakati
ya kutokomeza biashaara hiyo. Kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa
Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Mkurugenzi Mtendaji wa ANPPCAN
Tanzania, Wilbert Muchunguzi, akieleza jambo juu ya shughuli wanazofanya
katika kupambana na Biashara Haramu ya Kuzuia Usafirishaji Binadamu
nchini. Kushoto ni Katibu wa Kamati ya Kuzuia Usafirishaji Haramu wa
Binadamu, Seperatus Fella. Kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa
Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Mkurugenzi wa kituo cha C-sema,
Michael Kehongoh, akieleza jambo juu ya shughuli wanazofanya katika
kituo hicho kuunga mkono harakati za kupambana na Biashara Haramu ya
Kuzuia Usafirishaji Binadamu nchini. Kushoto ni Katibu wa Kamati ya
Kuzuia Usafirishaji Haramu wa Binadamu , Seperatus Fella. Kikao hicho
kimefanyika katika ukumbi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
No comments:
Post a Comment