• Breaking News

    ..

    ..

    Thursday, 10 August 2017

    RC MWANZA; AKICHUKUA KIWANDA CHA NGOZI


    Mkuu wa Mkoa Mwanza John Mongella leo August 10, 2017 ameamuru makampuni ya Skysraper na Caspian kurudisha funguo za kiwanda cha Ngozi Africa Tanneries Limied Mwanza kwa Serikali na kuwa mali ya Serikali rasmi.

    Kiwanda cha Ngozi Africa Tanneries ni miongoni mwa viwanda vilivyobinafsishwa wakati wa ubinafsishaji wawekezaji wake wakiwa Makampuni ya Skyscraper na Caspian lakini sasa kimefungwa baada ya wawekezaji hao kushindwa kuendeleza uzalishaji kwa muda mrefu na kuwa eneo la kutunzia vyuma chakavu.

    Kwa mujibu wa Bodi ya taifa takwimu mkoa wa Mwanza unaonesha unaviwanda vipatavyo1,470, huku viwanda vine vikiwa vimeajiri zaidi ya watu 500, saba vimeajiri watu kati ya 100 - 499, na viwanda vilivyo ajiri watu kati ya 50-99 vipo 8, viwanda vingine ni vile vilivyo ajiri kati ya watu 20-49 ambavyo idadi yake ni13, kwaupande wa viwnda vilivyo ajiri kati ya watu10-19 viwanda 22 na vile vilivyo ajiri kati watu ya 4-9 vikiwa ni viwanda 279 na mwisho kabisa ni viwanda vyenye watu kati ya 1-4 hivi jumla yake ni viwanda 1,074.

    Mwanza ni mmoja ya mikoa inayokuwa kwa kasi huku uchumi wake ukichangia kwa asilimia 9% katika pato la taifa yaani GDP

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI