• ..

    ..

    Thursday, 19 October 2017

    MBUNGE RITTA KABATI AMEKERWA NA MIMBA ZA UTOTONI KATIKA SHULE YA SEKONDARI YA KWAKILOSA


     Mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa kupitia chama cha mapinduzi (CCM) Ritta Kabati akiongea na wanafunzi,wazazi na walimu wakati wa mahafali ya kidato cha nne mwaka huu 2017 katika shule ya sekondari ya Kwakilosa iliyopo katika manispaa ya Iringa 
    Baadhi ya wanafunzi na wazazi walihudhuria sherehe za kuhitimu kwa wanafunzi wa kidato cha nne katika shule ya sekondari ya Kwakilosa iliyopo kata ya Mwangata.
    Mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa kupitia chama cha mapinduzi (CCM) Ritta Kabati akimkabidhi cheti mmoja ya wanafunzi wa kike aliyehitimu kidato cha nne katika shule ya sekondari ya Kwakilosa
    Na Fredy Mgunda,Iringa.
     
    Mbunge
    wa viti maalum mkoa wa Iringa kupitia chama cha mapinduzi (CCM) Ritta Kabati
    amekerwa na uwepo wa mimba za utotoni katika shule ya sekondari ya Kwakilosa
    iliyopo kata ya Mwangata manispaa ya Iringa kwa kuwa kitendo hicho
    kinachosababisha kushuka kwa elimu katika shule hii.
    Akizungumza
    wakati wa shererhe za kuhitimu elimu ya sekondari kwa wanafunzi wa kidato cha
    nne mwaka huu Kabati alisema kuwa amesikitishwa kusikia kila mwaka kuna
    wanafunzi wanakatisha masomo kwa ajili ya kupata ujauzito.
    “Jamani
    tumekuwa tukitoa elimu kila mara juu ya madhara yanayotoka na upatikanaji wa
    mimba za utoto za hiii shule imekuaje kila mwaka wanafunzi wanapata mimba hii
    haikubariki katika jamii kabisa maana hawa wanafunzi ndio tegemeo la taifa kwa
    sasa” alisema Kabati
    Kabati
    aliwataka wazazi na walimu kuwalinda wanafunzi wa kike ili wasikumbane na ardha
    ya kupata mimba wakiwa watoto wadogo kwani kunapoteza muelekeo wa maisha yao na
    maendeleo ya taifa kwa ujumla.
    “Haiwezekani
    kila mara wazazi mnakuwa wa kwanza kuwa chanzo cha kuwaharibu watoto na kwanini
    wazazi mnafanya hivyo maana watoto hawa ndio watakao wasaidia hapo baadae ndio
    maana mkiwa mmezeeka kwa hiyo ndio watakuwa msaada katika maisha yenu naombeni
    muwatunze watoto wenu” alisema Kabati
    Aidha
    Kabati aliwataka wanafunzi wote mkoani Iringa na Tanzania kwa ujumla kuacha
    kufanya mapenzi wakiwa na umri kama wao hivyo wanapaswa kujilinda ili kufikia
    malengo yao waliojiwekea na walidhike na kipato walicho nacho wazazi wao.
    “Hivi
    kaka mimi ningeanza mapenzi nikiwa na umri kama wenu unafikiri ningefikia
    malengo haya niliyonayo hivyo nawaomba msifanye mapenzi mkiwa na umri mdogo ili
    baadae mje kufikia malengo yenu” alisema Kabati
    Kwa
    upande wake mkuu wa shule hiyo Hudson Luhwago aliwatupia lawama wazazi na
    walezi wa wanafunzi wa shule hiyo kwa kutowalea katika malezi mazuri wanafunzi
    hao.
    “Yaani
    kabisa mzazi anakuja na wanafunzi anamuombea ruhusa kuwa walikuwa fiesta wote
    hivyo mtoto amechoka hawezi kuja shule hii ni aibu na ukweli unaoendelea kwa
    baadhi ya wazazi wa wanafunzi wa shule hii” alisema Luhwago
     Luhwago alisema kuwa kuna baadhi ya wanafunzi
    wanawanaume zaidi ya watano na wazazi wanayajua hayo lakini wanashindwa
    kuwakemea watoto wao na ndio maana wanakuja shule wakiwa na kiburi hata kwa
    walimu.
     
    “Wanafunzi
    hawa wanaomaliza hitimu shule leo walikuwa wanakiburi kwa sisi walimu hadi
    ikabidi tukae kama wanalimu tuwajadili lakini chanzo chote ni malenzi mabaya
    wanayoyapata kutoka kwa baadhi ya wazazi au walezi wao” alisema Luhwago
    Akisoma
    risala kwa mgeni rasmi makamu mkuu wa shule Praygod Makongwa alisema kuwa hadi
    sasa kuna mwanafunzi ameachishwa shule akiwa kidato cha kwanza kwa sasbabu ya
    kuwa mujamzito na hata hawa wanaohitimu hii leo mwenzao mmoja alikatisha masomo
    akiwa kidato cha pili kwa kuwa na ujauzito.
     
    “Sisi
    kama walimu wa shule hii tushazoe kuona wanafunzi wanakatisha masomo kwa ajili
    ya kupata mimba na ukiangalia kwa umakini walimu tunawalea wanafunzi kwa
    maadili yanayotakiwa tatizo lipo kwa wazazi hao unakuta mtoto na mzazi wapo
    disco pamoja wanakunywa pombe pamoja sasa hapo utapata matokeo gani?” alisema
    Makongwa
    Lakini
    Makongwa alisema kuwa shule imejiwekea mikakati ya kuhakikisha inajenga majengo
    ya mabweni kwa wanafunzi ili kumaliza tatizo la mimba za utoto na kuboresha
    elimu ya shule ya sekondari ya Kwakilosa.

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI