Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tamisemi, Suleiman Jaffo, amesema, bila
kusimamiwa kwa maadili katika jamii, taifa litashindwa kusonga mbele
katika juhudi za kujenga jamii inayochukia rushwa.
Akizindua
Maadhimisho ya Maadili ya Kitaifa Mjini Dodoma leo, Mh. Jaffo
amewakemea viongozi wote wanaokumbatia rushwa na kuziagiza mamlaka
zinazosimamia maadili kuwachukulia hatua kali ili kupunguza tatizo hilo
nchini.
Naye Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, CAG, Prof. Mussa
Assad, amesema, taasisi hiyo inaendelea kusimamia maadili na kupambana
na rushwa pamoja na kusimamia maadili na haki za binadamu, hivyo
kuendelea kuboresha ufanisi kwa jitihada za serikali.
Kauli mbiu ya maadhimisho hayo mwaka huu ni wajibika piga vita rushwa
zingatia maadili haki za binadamu na utawala bora kuelekea uchumi wa
kati.
No comments:
Post a Comment