Na stahmil Mohammed
Wafanyabiashara
wadogowadogo wanaofanya biashara kwenye stendi ya mabasi yaendayo
mikoani wamefanya maandamano madogo wakishinikiza na kupinga manyanyaso
dhidi ya wafanyabiashara huku lawama kubwa zikienda kwa meneja wa stendi
hiyo Imani E. Kasagala.
Akiongea
na wandishi wa habari katika mkusanyiko huo, katibu wa umoja wa
wafanyabiashara Ubungo John Shayo amesema kuwa walipewa idhini ya
kufanya biashara ndani ya stendi hiyo na meya ikiwa ni kuunga mkono
kauli ya Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania ya hapa kazi tu pamoja
na amri yake ya kuwaacha wafanyabiashara wadogowadogo kufanya
biashara kwa uhuru pasipo kubuguziwa.
Pia
Shayo ameongeza kuwa pamoja na tamko la Rais imekuwa tofauti kwa meneja
huyo kwani amekuwa na manyanyaso yasiyo na sababu za msingi na amekuwa
na kauli mbaya pindi wanapomuhitaji kwaajili ya mazungumzo hivyo
wanamuomba meya wa jiji kushughulikia tatizo hili ili waijue hatima yao
ni ipi
"Hili tatizo ni la mda mrefu hivyo tunamuomba meya wa jiji aje atoe tamko rasmi ili tujue hatima yetu ni IPI" amesema Shayo.
Pia
Shayo amesisitiza kuwa lengo lao ni kufanya kazi hivyo hawatayafumbia
manyanyaso ya meneja huyo hadi meya atakapokuja kufanya maamuzi tena
wakiwa pamoja na meneja huyo ili Haki itendeke.
"Lengo
letu ni kufanya kazi "hapa kazi tu" hivyo hatutakufumbia macho jambo
hili hadi meya atakapokuja kufanya maamuzi tena wakiwa pamoja na meneja
huyo ili Haki itendeke" amesema Shayo.
Aidha
pia mfanyabiashara mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Japhari Hatibu
ambaye ni mwenyekiti wa watembeza mikate ndani ya stendi amesema kuwa
wafanyabiashara wanapigwa faini bila kosa na hakuna lisiti inayotolewa
na anayeshindwa kutoa faini hupelekwa rumande.
Pia
Hatibu ameongeza kuwa pamoja na kutozwa faini pia Wapo wamama wajane
wanaotegemea biashara hiyo ili kulisha familia zao hivyo wanakuwa katika
wakati mugumu na itapelekea watu kujihusisha na biashara zisizofaa
endapo hali hiyo itaendelea.
Kwa
upande wake meneja kasagala aliyetupiwa lawama hizo amejibu tuhuma hizo
kwa kusema kuwa kituo kinaendeshwa na sheria ndogo ambayo marekibisho
wamefanya mwaka 2009 ambapo sheria hiyo ilikuwa inatumika toka mwaka
2004.
Akifafanua
sheria hiyo meneja huyo amesema kuwa biashara zozote zinazotembezwa
haziruhusiwi ndani ya kituo na kuongeza kuwa wanaoruhusiwa kuonekana
ndani ya kituo ni wanaohusika na mambo ya usafiri pamoja na wafanya
biashara wanaotambulika na wale walioko kwenye mfumo maalumu, kama vile
wenye maduka na wenye vibali maalum.
"Wanaoruhusiwa
kuonekana kwenye kituo ni wanaohusika na mambo ya usafiri pamoja na
wafanya biashara wenye vibali maalum na walioko kwenye mfumo maalumu
kama wale wenye maduka" amesema Kasagala.
No comments:
Post a Comment