
Na Stahmil Mohamed
Uongozi mpya Wa Jumuiya ya wazazi ya chama cha mapinduzi imeahidi kuimarisha umoja Wa jumuiya hiyo na kuifanya ya kujitegemea ili kufikia malengo ya jumuiya pamoja na nchi ya malengo ya uchumi Wa kati ambayo ni Sera ya serikali ya awamu ya tano Jamuhuri ya muungano Wa Tanzania ya Tanzania ya viwanda.
Hayo yamesemwa na Mwenyekiti Mpya Wa Jumuiya hiyo DKT
Edmund B Mndolwa baada ya kukabidhiwa rasmi Ofisi Leo na aliyekuwa
mwenyekiti Wa jumuiya hiyo ambaye kwasasa amemaliza mda wake DKT
Abdallah Bulembo ambapo DKT Mndolwa alianza Kwa kumshukuru Dkt Bulembo
Kwa kumkabidhi Ofisi rasmi Kwa maandishi na taratibu zote stahiki
ambapo amesema jambo hilo ni nadra sana kuona kwenye taasisi nyingine
hivyo hana budi kumshukuru Kwa ujasiri na uzingatiwaji wake Wa sheria
kwani anaamini jumuiya ya wazazi ni ya kwanza katika makabidhiano hayo .
Aidha DKT Mndolwa amesema atahakikisha anaimarisha umoja
Wa jumuiya hiyo ili izidi kuleta tija katika jamii pia atahakikisha
jumuiya inakuwa ya kujitegemea zaidi ili kufikia malengo ya Jumuiya na
kuepukana na hali ya kuombaomba katika chama ameongeza Kwa kusema kuwa
atahakikisha maadili ya watanzania yanakuwa kama miaka ya nyuma
ilivokuwa kama agizo la rais John pombe magufuli alivyoagiza kwenye
alipokuwa katika mkutano Mkuu wa Jumuiya ya wazazi uliofanyika Dodoma
hivo atahakikisha waanzia mashuleni kote kuwajenga kimaadili kwani huko
ndipo chimbiko la Taifa la Kesho linapoanzia.
Naye Makamu Mwenyekiti Wa jumuiya hiyo Haidal Haji Abdallah
amesema jumuiya itakimbizana na muda ili izidi kukua na kuimarika zaidi
Kwa upande wake DKT Bulembo wakati akimkabidhi Ofisi DKT
Mndolwa pamoja na vitendea Kazi vyote ikiwemo katiba ya chama,kanuni ya
Jumuiya na baadhi za Mali za jumuiya kama mashule,magari na kadha Wa
kadha pia DKT Bulembo ameahidi kushirikiana na uongozi huu mpya pindi
watakapohitaji ushirikiano Wa aina yoyote.
No comments:
Post a Comment