• Breaking News

    ..

    ..

    Tuesday, 2 January 2018

    Jimbo la Kinondoni linanisubiri

    Msanii wa filamu na mchekeshaji bongo ambaye pia ni kada wa chama cha Mapinduzi, Steve Mengere maarufu kama Steve Nyerere, ameonyesha nia ya kugombea ubunge wa jimbo la Kinondoni.
    Akizungumza na Big Chawa kwenye Planet Bongo ya East Africa Radio baada ya kuulizwa kama ana mpango wa kugombea ubunge, Steve Nyerere amesema yeye ndiye kijana ambaye anakubalika zaidi katika wilaya ya Kinondoni, hivyo anasubiriwa kugombea.
    “Wilaya ya Kinondoni unapozungumzia vijana ambao ni 'president' ni Steve Nyerere, ndio maana jimbo la Kinondoni linanisubiri mimi, we pita kila sehemu uliza tu utaambiwa”, amesema Steve Nyerere.
    Kutokana na hilo Steve Nyerere hatokuwa msanii wa kwanza kutangaza nia kwa jimbo la Kinondoni, kwani msanii wa muziki wa bongo fleva Khalid Mohamed maarufu kama TID, alishawahi kusikika akisema anakusudia kugombea ubunge wa jimbo hilo

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI