• Breaking News

    ..

    ..

    Wednesday, 3 January 2018

    Khafan ashinda nafasi ya unaibu meya wa jiji

    Image result for cuf zanzibarNa Stahmili Mohammed

    Uchaguzi wa kumpata naibu Meya wa jiji  la dar es salaam umefanyika Leo Mara baada ya jiji hilo kukaa pasipo kuwa na naibu meya takribani miezi sita.

    wagombea katika uchaguzi huo walikuwa ni Marian Ruida kutoka chama cha mapinduzi na Musa Khafana kutoka chama cha CUF ambapo katika idadi ya kura zilizopigwa na washiriki wa uchaguzi huo ni 22 huku kura 12 zilinyakuliwa na Mussa Khafana wa CUF na kura 10 zikiwa zimesalia kwa Mariam Ruida kutokea ccm.

    Hata hivyo Mara baada ya kutangazwa kwa matokeo hayo ya uchaguzi  mgombea kutokea ccm mhe.Mariam Ruida aliwashukuru wapiga kura na kuahidi kushirikiana na uongozi uliopo madarakani .

    Naye Said  Kubenea akizungumza kwa niaba ya mgombea wa CUF ambaye hali yake ya kiafya si nzuri  amesema wao kama Ukawa wanashukuru mungu kushinda nafasi hiyo licha ya kuwa mgombea wao hakuwa katika hali iliyopelekea wao kupitia changamoto mbalimbali hadi kufikia tamati ya uchaguzi.

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI