Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mwigulu Nchemba ameagiza
kukamatwa na kupimwa akili mtu anayejiita Nabii Tito na kuchunguzwa na
endapo itabainika kuwa ni mtu mwenye akili timamu kufikishwa kwenye
vyombo vya sheria.

"Nchi yetu hii tunaishi kwa kuheshimiana kwasababu tunaheshimu imani za watu ndio mana mpaka sasa bado tupo pamoja, wewe kama unajua wakristu wanaamini kama hakutakuwepo kanisa lipo kama baa au danguro wewe unaamua kutengeneza kanisa la aina hiyo au ndugu zetu waislam wao hawaamini katika Kitimoto wewe unaanzisha Msikiti ambao ukiingia tu unapewa Kitimoto huko ni kutengeneza chuki, uchochezi ambao unaweza kuleta uvunjifu wa amani" Mwigulu Nchemba
"Mtu huyu kwa sababu ni mtu mzima kwanza akamatwe apimwe akili vizuri na kama yupo sawasawa basi afike kwenye vyombo vya sheria, hauwezi kututengenezea vitu ambavyo vinaweza kuleta mapigano ya imani ndani ya nchi yetu, vita ya kiimani haina mshindi kwani mtu kwenye imani yake yupo tayari kufa, kama ni mgonjwa basi akatibiwe
No comments:
Post a Comment