
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe.Paul Makonda leo
amemsaidia Mama Mjane Bi.Benadetha Rwendela aliedhulumiwa Nyumba yake Plot No. 239 Block B Kunduchi Beach kwa kupigwa Mnada na Madalali
kutoka Kampuni ya Nkanya Ltd kinyume na taratibu kisha kuamrishwa kuondoka ndani ya siku 30.
Baada ya RC Makonda kuona taarifa hizo kwenye baadhi ya Vyombo vya Habari na Mitandao alimwita Mjane huyo Ofisini kwake kisha kumkutanisha na Wanasheria wa Mkoa na kubaini utapeli
uliotumika kuuza
Nyumba hiyo kutokana na watu kufoji nyaraka ikiwemo Sahihi ya Mwenyekiti wa Mtaa huku nyumba hiyo ikiwa Zuio la Mahakama.
Nyumba hiyo kutokana na watu kufoji nyaraka ikiwemo Sahihi ya Mwenyekiti wa Mtaa huku nyumba hiyo ikiwa Zuio la Mahakama.
Aidha imebainika Kuwa Hati za Nyumba hiyo zilifojiwa kisha
kutumika kuchukuwa Mkopo wa Shilingi Billion Moja pasipo mmiliki wa
nyumba kujua kinachoendelea.
Kutokana na hilo RC Makonda ameagiza Kamanda wa Polis
Kanda Maalumu ya Dar es Salaam LAZARO MAMBOSASA kuwakamata Matapeli
waliohusika pamoja kuagiza kusimamishwa Mnada huo kwakuwa ni batili
huku akimsihi Mama Mjane kuishi kwa Amani kwenye nyumba yake.
Aidha RC Makonda amesema Jumatatu ya wiki ijayo atakutana
na Bank ya KCB kwaajili ya Mazungumzo huku akiwaagiza Madalali wote
wanaotaka kufanya minada kwenye Mkoa huu kuhakikisha wanapata ruhusa
kutoka kwa Wakuu wa Wilaya.
Kwa upande wake Mjane huyo Bi. Benadetha Rwendela
ameishukuru Serikali ya awamu ya tano kwa kuwajali Wananchi wake na
kuwasaidia pale wanapopata matatizo huku akimpongeza Rais Magufuli kwa
kumteua RC Makonda.
No comments:
Post a Comment