• Breaking News

    ..

    ..

    Tuesday, 16 January 2018

    TAGCO kukutana machi 12-16 Arus


    Na Stahmili Mohammed.

    Mkutano mkuu wa chama cha maafisa habari Na mawasliano serikalini (TAGCO) kwa kushirikiana na idara ya habari maelezo habari, utamaduni na michezo  unatarajiwa kufanyika mnamo tarehe 12-16 machi mwaka huu mkoani Arusha ambapo jumla ya maofisa 300 wanatarajiwa kishiriki katika mkutano huo.

    Akiongea Na vyombo vya habari leo jijini dar es salaam mwenyekiti wa chama hicho Paschal Shelutete amesema kuwa lengo kuu kuelekea mkutano huo  ni kuweza kukumbushana wajibu na majukumu yao serikalini.

    Aidha amesema kuwa kikao hiko kina kazi ya kuwajengea washiriki uwezo wa namna ya kutangaza shughuli za serikali Na kuhakikisha idara ya mawasikiano Na uhusiano serikalini vinaimarishwa ili kuendana na kasi ya utendaji wa serikali ya awamu ya tano.

    Pia ameongeza na kusema kuwa katika mkutano huo jumla ya mada 14 zitaongelewa ambazo zitajikita zaidi kwenye masuala mbalimbali  yahusuyo habari, mawasiliano na itifaki.
    Pia amesema kuwa mada hizo zitawasilishwa na wataalam watakaoleta uzoefu mpana katika mawasiliano na kuongeza kuwa kutakuwepo mijadala na fursa ya kubadilishana uzoefu kati ya maaafisa mawasiliano na wadau wengine wa habari.

    Mwisho kabisa amewahasa maafisa habari, mawasiliano, uhusiano na itifaki kuthibitisha ushiriki wao kabla ya tarehe 7 machi mwaka huu.

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI