• Breaking News

    ..

    ..

    Monday 26 February 2018

    Serikali ya Tanzania yanyakua tuzo kutoka (WHO)

    Shirika la afya duniani (WHO) limetoa tuzo kwa serikali ya Tanzania kwa lengo la kuipongeza serikali hiyo kwa hatua waliyopiga katika udhibiti wa malaria kutoka asilimia 18% hadi kufikia asilimia 7.3%.

    Tuzo hiyo imepokelewa  na Mganga mkuu wa serikali prof.Mohamed Bakari wakati wa kikao kilicho wakutanisha wataalamu wa kudhibiti malaria duniani.

    Akizingumza Mganga mkuu wa serikali prof. Mohamed Bakari  amesema kuwa kikao hicho cha siku mbili kitajadili namna ya kupambana na kudhibiti kuenea kwa ugonjwa wa malaria kwa nchi nzima hasa katika mikoa inaoyoongoza  kwa ugonjwa wa huo nchini ikiwemo mikoa ya kanda ya ziwa ambayo ni kigoma, kagera , na geita.

    Kwa upande wa meneja mpango wa udhibiti malaria Dokt .Ally Mohamed  amesema kuwa serikali ya Tanzania inajivunia kuwa na kiwanda cha kutengeneza vyandarua vyenye dawa,pia ikiwa ni nchi ya kwanza kwa bara la Afrika kutoa vyandarua hivyo ambavyo vinadhibiti maambukizi ya malaria.

    Vilevile ameongeza kuwa shirika la Afya duniani  (WHO) limeipongeza serikali ya tanzania na wananchi katika hatua ya  kudhibiti kuenea Kwa ugonjwa wa malaria na ushirikishwaji wa mzuri  katika tafiti walizmbali walizokuwa wanashiriki.

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI