• Breaking News

    ..

    ..

    Thursday 24 May 2018

    Huu ndio ujumbe Wa RcMakonda



    Sio kila Mitihani Yote tunayopitia *MUNGU* hulenga kutupima sisi, mara nyingine *MUNGU* hutupa sisi mitihani ili kupima *imani* za wale *wanaotuzunguka* katika maisha yetu.

    Siku moja nilipokuwa *katikati* ya vita kali, *nakumbuka* ilikuwa mwaka jana ambapo kila aina ya *mshale* niliuona, na katika *kutafakari* nilijiona kama msafiri nilieko ndani ya *mtumbwi* uku nikitegemea *mshumaa* kama taa hali ya kuwa *Dhoruba* kali na upepo *vikipiga* huku matumaini yangu yakiwa ni kuvuka kwa *kutumia* Mwanga wa *Mshumaa,* sio rahisi wakati *mwingine* kujua ilikuwa ni *ngumu* kiasi gani, na hapo ndipo *nilipofanikiwa* kuwaona wengi kwenye *Sura* halisi na *hulka* ambazo sikuwahi *kuzitegemea* juu *yangu.*

    Nikiwa *natafakari* safari yangu, bado uku *Dunia* nzima ikiwa imenigeuka, kama *MUNGU* tu ndipo pale niliponena na *mtumishi* mmoja ambae ni *KIONGOZI* WANGU akaniambia neno moja *"USITAKE SUPPORT YA WANAADAMU, MUNGU AKIKUSUPPORT INATOSHA* "

    Sikuwahi kupata *faraja* kubwa kama *nilivyoipata* kupitia neno hilo na nitamshukuru *Daima,* na hapo ndipo nilipoanza kutafakari kisa kati ya *BAHARI NA SWIMMING POOL.*

    Ukiiangalia *BAHARI,* miaka nenda rudi huwa ipo tu pale na haijawahi kuisha *matumizi* yake, pamoja na kuwa haina uangalizi wa aina yoyote Lakini thamani yake haijawahi *kushuka* ,Inaongezeka *Kila* Siku *haikauki* huku maji yake yakiendelea kutumika bila shaka wala wasiwasi

    Bahari hata itupiwe *UCHAFU* wote wa nchi kavu bado haibadilishi chochote kwenye *UBORA* wake sababu imeshaumbwa hivyo na mwenye *KUWEZA,* haijatengenezwa na Mwanadamu ila *IMEUMBWA* na *MUNGU.*

    Ukirudi kwenye Upande wa *SWIMMING POOL* pamoja na kuzitengeneza kwa *Urembo* na maumbo tofauti tunayoyataka *SISI* huku gharama kubwa ikitumika, lakini bado ili iendelee kuwepo inahitaji *Matunzo* mengi na uangalizi wa hali ya juu otherwise ikiachwa hata kwa siku chache tu itageuka *BWAWA CHAFU* na kila mtu ataogopa kutia *Mguu* wake, hata utunzaji wake inabidi uwe makini sana sababu *SIO NATURAL,* uchafu unaobebwa na *Bahari* ukiutia kwenye pool hata kwa siku moja tayari ni doa *KUBWA* , hivyo maisha yote ni ya kushikwashikwa na *KUBEBWABEBWA* ili iendelee kutazamika.

    Hata Binaadamu tuko hivyo katika vile vilivyowekwa ndani mwetu na ni MUNGU tu anaeamua, kuna wale ambao ni BAHARI na kuna wale SWIMMING POOL , na kwa bahati mbaya waliopewa na MUNGU wanaonekana na wengine wanajulikana, na zaidi kilichojengwa na Binaadamu always kina expiring date hata kiwe kwenye umbo zuri kiasi gani hakitakuwa na UHAI wa moja kwa moja tofauti na kilichowekwa na MUNGU kitadumu milele.


    Kitu kinachonipa moyo wa kusonga kwenye maisha yangu ni kwakuwa I am not MAN MADE, I am GOD GIFTED, na kutoka moyoni najiona kama mfano wa bahari.

    Hivyo ukiwa BAHARINI usiwe na shaka, hata ubebe uchafu wa dunia nzima bado thamani yako itabaki Palepale na kila mtu ataihitaji, life is there for you, HAKUNA WA KUKUSHUSHA sababu kuna aliekutengeneza anaezidi maarifa wote.

    Naandika Mawazo haya nikiwa katika mlima Sinai, nikiwa natafakari kuhusu haya ningependa ujitafakari na wewe kuhusu kundi Ulilopo.

    Nikiwa natafakari Haya katika Mlima Sinai, Naomba ujiulize na wewe Ukokatika Kundi Gani?

    Ni Mimi Mtumishi wa Mungu

     Paul Makonda

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI