• Breaking News

    ..

    ..

    Tuesday 22 May 2018

    Watoa huduma za maabara wametakiwa kufuata taratibu za usajili ili kutoa huduma kwa wagonjwa

    Mkurugenzi Msaidizi huduma za uchunguzi wa Wagonjwa Wizara ya Afya Dkt. Charles Massambu amewataka waajiri na Waajiriwa wanaotoa huduma za Maabara kuhakikisha wamesikilizwa na  wanafuata taratibu za usajili na kwa yeyote atakayebainika hajafuata taratibu hizo atachukuliwa hatua za kisheria.

    Hayo ameyasema leo katika semina fupi ya waandishi wa habari jijini Dar es salaam ambayo imelenga kuwajengea uwezo waandishi wa habari  juu ya  huduma za maabara.

    Amesema  Massambu changamoto  zinazoikabili Baraza la Maabara la niwatoa huduma za Maabara  na Wataalamu kutoa huduma pasipo kusajiliwa na kukosa leseni ambapo ni kosa la  jinai kisheria.

    Kwa upande wake Msajili Baraza la afya Theophil Mabiliche amesema baraza linafanya juu chini ili kubaini wanaogushi vyeti frki na mpaka Sasa wamefanikiwa kubaini watu 71 waliogushi vyeti na wanajitahidi kufanya msako Kwa wanaogushi vyeti ili kusaidia wagonjwa kupata huduma ipasavyo.

    Aidha amesema Mtaalamu yeyote haruhusiwi kuendesha Maabara ambayo haijasajiliwa kisheria na haruhusiwi Mtaalamu kutoa taarifa ya mgojwa ya majibu ya vipimo vyake bila utaratibu pasipo ruhusa ya mgonjwa au ndugu wa mgonjwa.

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI